Search This Blog

Wednesday, 28 January 2015

AHADIWAY NI NINI?

AHADIWAY NI NINI?
Ni asasi isiyo ya kiserikali inayoshughulika hasa na masuala ya kijamii.
Asasi hii ilisajiliwa rasmi tarehe 06 Januari 2014 chini ya kifungu cha sheria 12(2) ya 2002 (The None Government Organisation Act)  Asasi hii imejikita katika mchakato wa kupunguza umaskini  kwa kuwapatia watanzania wote mbinu za kuweza kupambana na umaskini.
WALENGWA NI AKINA NANI?
Kila mtanzania aliyefikisha umri wa miaka kumi na nane na kuendelea aliye tayari kubadilika kimtazamo na kuukataa umaskini.
NAWEZAJE KUWA MWANACHAMA WA AHADIWAY?
Ili uwe mwanachama wa Ahadiway unapaswa uwe katika kikundi cha watu watano ( 5) mpaka kumi na tano (15) mliokubaliana kuungana . Gharama za kujiunga kama kikundi ni sh laki tatu (300,000) Pesa hii itatumika katika usajili wa kikundi hicho kama kampuni itakayotambuliwa na BRELLA. Cheti hicho kitasaidia kikundi katika kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuaminika kukopeshwa pesa kutoka taasisi za fedha,

FURSA ZIPATIKANAZO AHADIWAY.
Kama taasisi inayojishughulisha na mkakati wa kupunguza umaskini  Ahadiway imeandaa fursa nyingi apatazo mwanachama wake
Ø Kupata mikopo  ya fedha taslimu
Ø Mikopo kwa ajili ya Miradi Mikubwa
Ø Mikopo ya bajaji zinazotumia umeme
Ø Mikopo ya magari
Ø Mikopo ya nyumba za bei nafuu

MIKOPO YA FEDHA TASLIM.
Mwanachama akishajiunga anatakiwa kuanza kujiwekea akiba ambayo tunaita HISA. Utaratibu  wa kuweka hisa utamsaidia kukopa `mara mbili pindi atakapofikisha zaidi ya miezi mitatu. Anachotakiwa kufanya ni kujaza fomu ya mkopo na kueleza kusudi la mkopo na pia fomu yake lazima isainiwe na wadhamini wanne ambao ni wanachama wenye hisa za kutosha ili mkopaji akishindwa kulipa kwa muda uliopangwa ,hisa zake na za wadhamini wake zitakatwa ili kufidia deni lake.

MIKOPO YA MIRADI MIKUBWA.
Mikopo ya miradi mikubwa ni mikopo itakayotolewa kwenye kikundi baada ya kukamilika kwa taratibu zote za usajili. Wanakikundi wanatakiwa kuandaa mchanganuo wa biashara wanayohitaji kuifanya. Mchanganuo huo wa biashara utawasilishwa makao makuu kwa ajili ya kuufanyia kazi. Endapo kama kutakuwa na gharama zozote kwa ajili ya ule mchanganuo, wanakikundi watapewa taarifa ili kulipia hizo gharama. Kiwango cha mkopo wa mradi kitategemea na aina ya mradi ulioombewa pesa hata kama ni milioni mia moja.
Pesa za miradi zinatoka katika taasisi za fedha ambazo tumeingia nazo mkataba kwa ajili ya wanachama wetu, hata viwango vya riba vitatokana na aina ya mkopo uliotolewa.

BAJAJI ZA UMEME.
Hizi ni bajaji za aina yake ambazo hutolewa na Shirika la Ahadiway pekee. Bajaji hizi hukopeshwa kwa mwanachama yeyote ili mradi akidhi vigezo na masharti. Kikundi au mwanachama mmoja mmoja anaruhusiwa kukopa bajaji’ Anachotakiwa kufanya ni kutanguliza milioni mbili (2,000,000) kama kianzio kisha anapewa bajaji yake. Mwezi mmoja baada ya kuchukua bajaji anatakiwa kuanza kurejesha deni lake kwa kipindi cha miezi minane. Gharama ya bajaji hizo ni sh milioni sita tu.
Mikopo ya magari bado tunaifanyia kazi.


MIKOPO YA NYUMBA ZA BEI NAFUU.
Tunawasiliana  na mashirika yanayojenga nyumba na kuwapatia wanachama wetu fursa za nyumba za bei nafuu  kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.hata hivyo ahadiway itaanza kujenga nyumba  kwa ajili ya wanachama wake tuu ili kuhakikisha kwamba kila mwanachama anapata nafasi ya kuishi katika nyumba bora.

HISA ZA AHADIWAY.
Hisa ni akiba au amana ambayo mwanachama atawekeza Ahadiway ili kumuwezesha kuaminika  na kumjengea mazingira mazuri ya kukopesheka.

UNUNUAJI WA HISA.
Wanakikundi wanahimizwa kukutana mara kwa mara kwa lengo la kununua hisa zao ambazo kima cha chini ni sh 2000 na kiwango cha juu hutegemea na mwanachama mwenyewe jinsi alivyodhamiria kupambana na umaskini. Hisa zinaweza kununuliwa mara moja kwa wiki, mara mbili kwa mwezi au mara moja kwa mwezi kutegemeana na ratiba ya wanakikundi wenyewe. Hisa zote zitawekwa benki kwenye akaunti ya Ahadiway Hisa Account

 

FAIDA ZITOKANAZO NA HISA.
Hisa yako itakusaidia kupata mkopo wa fedha taslim ambao ni mara mbili ya hisa zako.
Kila baada ya mwaka mmoja baada ya kununua hisa utapata gawiwo au faida ya asilimia ishirini ya hisa zako au thamani ya kiwango cha faida iliyo patikana.
Pamoja na hayo hisa itakuwezesha kuaminika na Ahadiway katika kutafutiwa fedha za miradi unayotaka kuifanya.

MATARAJIO YETU.
·       Wanachama wote wa Ahadiway wanatimiza ndoto zao
·       Kufikia mwisho wa mwaka kila kikundi kiwe kimeshapata mradi mkubwa wa pamoja
·       Wanachama wote tutakuwa tumepunguza umaskini kwa kiwango kikubwa

·       Wanachama wote tutakuwa na furaha na amani tele.
Tunahitaji kila mtanzania apate nafasi ya kufanya kazi kwa hali yoyote na kwa kiwango chochote.
tunatoa mafunzo ya aina mbalimbali ili kuhakikisha walengwa wanapata huduma na fursa zote wanazoweza kuzifikia kwa uwezo wao au kwa msaada kutoka ahadiway.
akiba yako maendeleo yako.

Thursday, 1 January 2015

Employment training( fursa za mikopo na biashara kubwa) mnakaribishwa kiingilio ni bureee

GOOD NEWS, GOOD NEWS, GOOD NEWS!
 Life after school training 

Fursa za kazi kwa vijana waliopo vyuoni na waliomaliza. Life after school training  Ahadiway life development initiative imeandaa mafunzo na fursa za wanafunzi waliopo vyuoni na waliomaliza kuwawezesha kupata kazi mara baada ya kumaliza masomo. Ahadiway imeandaa mafunzo ya ajira na kujiajiri na kujitambua na kukuwezesha kuwamstari wa mbele katika maendeleo. Ahadiway itahakikisha kila mhitimu na yule aliopo chuoni kupata mafunzo na nyenzo za kazi atafanikiwa. Njoo upate nafasi ya kujiandaa na maisha ya sasa na baada ya chuo na jinsi gani unaweza kuyaandaa bado ukiwa chuoni. Njoo kwenye mafunzo hayo bila kukosa. Hakuna kiingilio. Yatafanika jumapili ya tar 04/01/2015 kuanzia saa 8 mchana hadi saa 10 tupo karibu na ofisi za itv wanaporushia matangazo  mwenge Dar es salaam. Msikose kufika ukipata ujumbe huu mjulishe mwenzako. . Wasiliana kwa number zifuatazo 0655490254 au 0789273938 au tembelea http://ahadiway.blogspot.com/  au https://www.facebook.com/pages/Ahadiway/539124546128964